WANAFUNZI WA STASHAHADA YA UALIMU WA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI UDOM KUNUFAIKA NA MIKOPO YA ELIMU YA JUU

M kurugenzi Msaidizi Habari, Elimu na Mawasiliano toka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Bw. Cosmas Mwaisobwa akiongea na waand...

Mkurugenzi Msaidizi Habari, Elimu na Mawasiliano toka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Bw. Cosmas Mwaisobwa akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu maandalizi ya utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2014/2015, wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa.


Frank Mvungi_ Maelezo
Serikali  imetoa fursa ya mikopo kwa wanafunzi watakaojiunga na masomo ya stashahada maalum ya ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari Elimu na Mawasiliano toka Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu Bw. Cosmas Mwaisobwa wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari Leo Jijini Dar es salaam.
“ Wanafunzi wapatao 5,000 wanatarajiwa kujiunga na stashahada maalum katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambapo wote watanufaika na mikopo ya elimu ya Juu.”Alisema Mwaisobwa
Akifafanunua, Mwaisobwa alisema kuwa lengo la mpango huo ni kusaidia kuondoa tatizo la walimu wa masomo ya sayansi hapa nchini .
Aidha Mwaisobwa alibainisha kuwa jumla ya maombi 58,037 ya mikopo  yalikuwa yamepokelewa hadi kufikia Julai 2014 ambapo maombi 37,689 ni waombaji wa kiume na 19,592 ni waombaji wa kike.
Pia Mwaisobwa alibainisha kuwa majina ya wanafunzi watakaopata mikopo kulingana na udahili yatatangazwa kwenye tovuti ya Bodi  ambayo ni www.heslb.go.tz .na taarifa hiyo itatangazwa katika vyombo vya habari.
Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB) inakusanya wastani wa shilingi bilioni 3 kwa mwezi ikiwa ni marejesho ya mikopo iliyokwisha tolewa.

Related

BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU (HESLB) YATOA KAULI KUHUSIANA NA KUCHELEWESHWA KWA POSHO YA MAFUNZO KWA VITENDO

Bodi ya mkopo ya Elimu ya Juu nchini Tanzania (HESLB) inashughulikia tatizo la wanafunzi wanaokwenda kwenye mafunzo kwa njia ya vitendo ikiwa na baada ya kulalamikiwa na jumuiya ya wanafunzi wa...

MAJINA YA VIJANA KIDATO CHA SITA 2014 MUJIBU WA SHERIA AWAMU YA PILI NA VIKOSI WALIVYOPANGIWA (JKT)

VIJANA WA KIDATO CHA SITA 2014 MUJIBU WA SHERIA AWAMU YA PILI(Bofya kwenye vikosi hapo chini kuangalia majina) BULOMBORA - KIGOMA RWAMKOMA - MUSOMA MSANGE - TABORA KANEMBWA - KIGOMA RU...

MAJINA YA WALIMU NGAZI YA CHETI 2014 MUJIBU WA SHERIA NA VIKOSI WALIVYOPANGIWA (JKT)

WALIMU-CHETI KWENDA VIKOSI MBALIMBALI(Bofya kwenye vikosi hapo chini kuangalia jina) BUROMBOLA - KIGOMA RWAMKOMA - MUSOMA MSANGE - TABORA KANEMBWA - KIGOMA RUVU - PWANI OLIJORO - ARUSHA...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item