AJIFUNGUA PACHA WA KIKE WALIOUNGANA SEHEMU YA KIFUA, TUMBO

    MUSOMA. Mwanamke mmoja mkazi wa Kata ya Buhare, Manispaa ya Musoma mkoani Mara, Helena Paulo (20), amejifungua watoto pacha w...


 
 MUSOMA.
Mwanamke mmoja mkazi wa Kata ya Buhare, Manispaa ya Musoma mkoani Mara, Helena Paulo (20), amejifungua watoto pacha wa kike walioungana eneo la kifuani hadi tumboni wakiwa na uzito wa kilo 4.6 kwa pamoja.
Tukio hilo la ajabu katika Mji wa Musoma na mkoa kwa jumla, liliwavutia hisia za wananchi hali iliyosababisha msongamano katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa madhumuni ya kutaka kushuhudia.
 
Akizungumza katika wodi ya wazazi hospitalini hapo, muuguzi wa zamu, Naabu Geraruma alisema mwanamke huyo alijifungua juzi saa saba usiku kwa njia ya upasuaji.
Geraruma alisema tukio hilo ni la kwanza katika hospitali hiyo na hali ya afya ya mzazi huyo na watoto inaendelea vizuri na muda wowote atahamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza.

Kwa upande wake, Mganga wa Idara ya Magonjwa ya Wanawake, Dk Simon Kamuli alisema baada ya jitihada za kuhakikisha mwanamke huyo anajifungua salama kukamilika, kinachofuatia ni kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa uangalizi zaidi.

Alisema kuwa hospitali ya mkoa haina uwezo wa kuwafanya chochote watoto hao, ikiwamo kuwatenganisha na taratibu zingine kabla ya uchunguzi wa kina.
MWANANCHI

Related

TUJUZANE 1870934645533163077

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item