NAIBU WAZIRI WA NISAHATI NA MADINI AKUTANA NA MAMENEJA WA TANESCO,MKOA LINDI, MTWARA, PWANI NA DAR ES SALAAM

  Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (katikati) akiwa katika kikao kilichojumuisha watendaji wa TANESCO, REA, na wak...


 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (katikati) akiwa katika kikao kilichojumuisha watendaji wa TANESCO, REA, na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Kulia kwa Waziri ni, Mhandisi Nishati Mwandamizi, kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Salum Inegeja na kushoto ni Mhandisi Thomas Visi, Meneja wa kampuni ya Naomis Corporate Ltd inayotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini katika mkoa wa Mtwara. 

  Mhandisi Mkuu Usambazaji Umeme katika mikoa ya Dar es Salaam, Benedict Lyaruu (wa kwanza kulia), Kaimu Meneja wa TANESCO, mkoa wa Pwani, Eng. Rehema Mashinji (katikati) na Mhandisi Miradi ya Umeme katika mkoa wa Pwani, Leo Mwakatobe (kushoto) wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (haonekani pichani) wakati wa kikao chake na watendaji wa TANESCO, REA, na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika miko ya Lindi na Mtwara. 

  Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (mbele, katikati) akiwa katika kikao kilichojumuisha watendaji wa TANESCO, REA, na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Kulia kwa Waziri ni, Mhandisi Nishati Mwandamizi, kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Salum Inegeja (kulia) na kushoto ni Mhandisi Thomas Visi, Meneja wa kampuni ya Naomis Corporate Ltd inayotekeleza miradi ya usambazaji umeme katika mkoa wa Mtwara.

 Mhandisi Miradi ya Umeme katika mkoa wa Pwani, Leo Mwakatobe (aliyesimama) akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya usambazaji umeme katika mkoa wa Pwani mbele ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (haonekani katika picha). Wa kwanza kulia mstari wa mbele, ni Meneja Mwandamizi wa TANESCO, Kanda ya Dar es salaam na Pwani inayojumuisha mikoa ya Lindi na Mtwara, Mhandisi Mahende Mugaya na wengine ni watendaji wa TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini. 

 Meneja wa TANESCO mkoa wa Lindi, Mhandisi John Bandiye akitoa taarifa ya miradi ya usambazaji umeme vijijini katika mkoa wa Lindi, mbele ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (haonekani katika picha).Wengine katika picha ni watendaji wa TANESCO kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara na Pwani.

Related

OTHER NEWS 7080818569895418378

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item