Amani yaanza kutengamaa Sudan Kusini

Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Salva Kiir amemtumia ujumbe Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya y...


Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Salva Kiir amemtumia ujumbe Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akimuarifu kuwa hali ya usalama katika nchi hiyo imeanza kutengemaa.

Rais Salva Kiir Mayardit amewasilisha ujumbe huo kupitia kwa Mjumbe wake Maalum Mhe. Aggrey Tisa Sabuni ambaye pamoja na kuwasilisha ujumbe huo amesema Sudani Kusini imekamilisha nyaraka za azimio la kuridhia mkataba wa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao umewasilishwa tarehe 05 Septemba, 2016 katika makao makuu ya Jumuiya Jijini Arusha. 

Mhe. Aggrey Tisa Sabuni amesema Sudan Kusini ipo tayari kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika masuala mbalimbali yenye manufaa kwa wananchi ikiwemo biashara na uwekezaji na kwamba ni matumaini yake kuwa itapata ushirikiano mzuri.

Kwa upande wake Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa kwake na taarifa za kutengemaa kwa hali ya amani nchini humo na kwamba ni matarajio yake kuwa Sudan Kusini itajikita katika maendeleo ya wananchi wake.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amepokea ujumbe kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza ulioletwa na Mjumbe Maalum wa Rais huyo Mhe. Aime Laurentine Kanyana.Katika ujumbe huo Rais Nkurunziza amesema hali ya Burundi ni shwari na kwamba wananchi wa Burundi wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.

Kwa upande wake Rais Magufuli amesema Tanzania yenye wakimbizi takribani 200,000 wa kutoka Burundi inafurahishwa na taarifa za kuwepo hali ya amani nchini humo.

Related

BOTI YA KILIMANJARO MALI YA AZAM MARINE YAPATA AJALI IKITOKEA PEMBA, MAITI 5 ZAPATIKANA

Boti ya Kampuni ya Azam Marine ya Kilimanjaro  ikitokea Pemba asubuhi ya leo ikiwa na abiria karibu 320 imepata misukosuko ya hali ya upepo na mawimbi na kusababisha baadhi ya abiria wali...

MOTO ULIVYOITEKETEZA JANCO MOTEL ILIYOPO MBEYA JANA USIKU

Jana usiku moto mkubwa ulizuka katika hotel ya Janco iliyopo eneo la Forest Mpya na kuteketeza baadhi ya vitu, chanzo cha moto huo hakijafahamika hadi sasa. Idadi ya vifo na ma...

MFANYABIASHARA WA KIKE APIGWA RISASI USONI NA KUPORWA MABEGI MAWILI YA FEDHA KARIAKOO.

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA Mwili wa mfanyabiashara huyo ukiwa kwenye gari mara baada ya kupigwa risasi na majambazi (majira ya saa 12 Kasoro jana jioni) Damu ya Mfanyabiashara huyo ikiwa im...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904812
item